Pages

Pages

Pages

Tuesday 8 September 2015

RAIS BUHARI ALISIFU JESHI LAKE

Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari, amesema kikosi chake cha ulinzi kimepata mafanikio katika mapambano yake dhidi ya wanamgambo wa Boko Haram.
Katika mahojiano na BBC, Rais Buhari amesema malengo yake ni kuona kwamba wapiganaji hao wa kiislamu hawajiimarishi na kuteka miji na vijiji.
Mwezi uliopita Buhari aliahidi kuwashinda wanamgambo hao wa Boko Haram ndani ya miezi mitatu.
Amefahamisha pia kwamba kundi la watu lililotekwa na Boko Haram katika msitu wa Sambisa limegunduliwa lakini bado haijafahamika wazi kama kati ya hao ni wanafunzi wa kike waliotekwa kutoka Chibok mwaka uliopita.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment