Pages

Pages

Pages

Wednesday 19 August 2015

MAN UNITED YAICHAPA CLUB BRUGGE KATIKA MCHUJO WA UEFA

Marouane Fellaini akipongezwa baada ya kufunga bao la ushindi kwa Manchester United
Manchester United imeanza vizuri mchezo wa kwanza wa mchujo kuwania nafasi kuingia hatua ya makundi ya michunao ya klabu bingwa barani Ulaya baada ya kupata ushindi wa 3-1 dhidi ya Club Brugge ya Ubelgiji .
Brugge ilipata bao lao mapema dakika ya 8 ya mchezo baada ya kiungo wa Man U Michael Carrick kujifunga.
Mshambuliaji mpya wa kikosi hicho cha mashetani wekundu Memphis Depay akasawazisha bao hilo dakika ya 14 kabla ya kuongeza bao la pili dakika 43, kiungo aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Wayne Rooney, Mbelgiji
Marouane Fellaini, akifunga bao la tatu lilihitimisha ushindi huo.
Matokeo mengine ya michezo ya mchujo kuwania kuingia hatua ya makundi ya klabu bingwa ulaya ni:
Astana 1 APOEL Nicosia 0
BATE Borisov 1 Partizan Belgrade 0
Lazio 1 Bayer Leverkusen 0
Sporting CP 2 CSKA Moscow 1
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment