Pages

Pages

Pages

Thursday 18 June 2015

SHAMBULIO LA KANISANI LAUA 9 MAREKANI


South Carolina
Polisi katika jimbo la South Carolina nchini Marekani wamesema kuwa mtu mmoja aliyejihami kwa bunduki amewapiga risasi na kuwaua watu tisa ndani ya kanisa la kimethodist.

Polisi wa eneo hilo la Charleston wameelezea kuwa kwa sasa wanamtafuta mshukiwa huyo anayeaminiwa kuwa kijana wa kizungu katika miaka ya ishirini.
Shambulio hilo limefanyika ndani ya kanisa la Emmanuel African Methodist Church, kanisa linaloaminiwa kuwa la zamani zaidi la kiafrika nchini Marekani
Polisi wamesema kuwa shambulio hili ni la chuki ya rangi ya ngozi.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment