Pages

Pages

Pages

Friday 19 June 2015

LIGI YA WANAWAKE DAR YASUBIRI RATIBA YA TWIGA STARS

Ligi ya wanawake mkoa wa Dar es salaam iliyomaliza mzunguko wake wa kwanza,ipo katika maandalizi ya kuanza mzunguko wa pili na wa mwisho kumpata bingwa wa ligi hiyo.
Kamati ya mashindano ya DRFA,imesema kinachosubiriwa kwa sasa ni ratiba ya benchi la ufundi la timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars,ambao wapo kambini kujiandaa na michuano ya afrika (All African Games) huko Congo Brazavile,mwezi Septemba mwaka huu.
Mpaka sasa kikosi cha Mburahati Queens ndicho kinachoshikilia usukuni wa ligi kwa kuwa na pointi 18,nafasi ya pili inashikiliwa na Evergreen Queens wenye pointi 12,sawa na JKT Queens wenye pointi 12 katika nafasi ya tatu wakitofautiana magoli.

No comments:

Post a Comment