Pages

Pages

Pages

Sunday 28 June 2015

HATARI: WANAWAKE WAJITOA MUHANGA NIGERIA, WAUA WATATU


Wanawake wawili washambuliaji wa kujitoa muhanga wamewaua takriban watu watatu kwenye shambulizi katika mji wa Maiduguri ulio kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Wanawake hao walijaribu kuingia kwenye hospitali lakini wakasimamishwa na walinzi langoni ambapo walijilipua.
Watu wengine 16 walijeruhiwa.
Shambulizi hilo ndilo la hivi punde kati ya mashambulizi yanayoendeshwa na wanamgambo wa Boko Hara.
Rais mpya wa Nigeria Muhammadu Buhari ameufanya mji wa Maiduguri kuwa kituo cha kijeshi kuweza kupambana na Boko Haram.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment