Pages

Pages

Pages

Sunday 24 May 2015

RIO FERDINAND AZUNGUMZA KWA MARA YA KWANZA BAADA YA KIFO CHA MKEWE

Rio Ferdinand
Aliyekuwa Nahodha wa timu ya soka ya Uingereza Rio Ferdinand amezungumza kwa mara ya kwanza tangu kifo cha mkewe kilichosababishwa na saratani na kusema kuwa ulikuwa wakati mgumu katika maisha yake.

Akiandika katika gazeti la the sun, aliusifu ujasiri wa mkewe Rebecca Ellison ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 34 mapema mwezi huu.
Mlinzi huyo wa kiabu ya QPR pia alisema kwamba alihisi kufanya makosa wakati alipokosa baadhi ya mechi wakati timu yake ilipokuwa ikijaribu kuzuia kushushwa daraja.
Rio Ferdinand na marehemu mkewe
Mkewe ambaye alimuoa mwaka 2009 ,alifariki May mosi kutokana na saratani ya matiti.
Amewaacha watoto watatu ,Lorenz mwenye umri wa miaka tisa,Tate mwenye umri wa miaka sita na Tia mwenye umri wa miaka minne.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment