Pages

Pages

Pages

Tuesday 26 May 2015

EBOLA: WATU SITA WAWEKWA KARANTINI JELA GUINEA

Guinea bado inapambana na Ebola
Watu sita wamewekwa karantini gerezani nchini Guinea baada ya kushutumiwa kusafiri wakiwa na mwili wa mtu aliyekufa kwa ugonjwa wa Ebola.

Mamlaka zinasema mwili huo ulikalishwa wima kwenye Taxi mithili mtu aliye hai, ukiwa umevaa T-shirt na Suruali aina ya Jeans na miwani ya jua akiwa kati kati ya Watu wengine wawili.
ikiwa baada ya siku 21 hawataonyesha dalili yeyote ya kuwa na Virusi vya Ebola watafikishwa mahakamanni kwa makosa ya kukiuka sheria za maswala ya afya.
Guinea iko kwenye Kampeni ya kutokomeza ugonjwa wa Ebola.
Takriban watu 2,500 wamepoteza maisha nchini Guinea tangu ugonjwa huo ulipokumba Afrika Magharibi zaidi ya mwaka mmoja uliopita.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment