Pages

Pages

Pages

Wednesday 6 May 2015

BABU AMCHOMA MKEWE MWENYE UMRI WA MIAKA 16!


Mzee mmoja mwenye umri wa miaka 70 aliyemchoma mkewe mwenye umri wa miaka 16 mjini Mandera kazkazini mashariki mwa Kenya amekamatwa.

Mke huyo aliyelazimishwa kuingia katika ndoa mwaka 2014 amelazwa katika hospitali kuu ya Mandera akiwa na majeraha mabaya ya kifuani pamoja na mikononi, kiongozi mmoja wa wanawake Ubah Gedi amethibitisha.
Mwanamke huyo sasa tayari amesafirishwa hadi jijini Nairobi kwa matibabu zaidi.
Ufichuaji huo uliofanywa kuhusu shambulizi hilo ni wa kushangaza kwa kuwa maswala mengi ya kijinsia Kazkazini mwa Kenya yameendelea bila kuripotiwa.
CREDIT: BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment