Pages

Pages

Pages

Monday 6 April 2015

NDEGE ZA DHARURA KUSAMBAZA DAWA YEMEN

 
Shirika la Kimataifa la Msalaba mwekundu limesema linamatumaini ya kupeleka ndege mbili za dharura katika mji mkuu wa Yemen Sanaa.

Shirika hilo la Msalaba mwekundu limesema limepewa ruhusa na Muungano wa jeshi linaloongozwa na Saud Arabia, kutua na ndege zilizobeba wafanyakazi na dawa zitakazosambwazwa nchini humo.
Jeshi hilo la Saudia linaongoza kampeni ya kupambana na waasi wa Houthi.
Kusini mwa Yemen waasi hao wa Houthis wameweza kuongeza nguvu katika mji wa Aden dhidi ya majeshi yaliyotiifu kwa rais wa nchi hiyo Abdrabbuh Mansour Hadi, licha ya mashambulizi ya anga yanayofanywa na majeshi hayo ya muungano.
CREDIT: BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment