Pages

Pages

Pages

Wednesday 15 April 2015

MUDA WA KUPIGA KURA WAONGEZWA SUDAN

Uchaguzi nchini Sudan
Tume ya uchaguzi nchini Sudan inasema kuwa imeongeza mda wa kupiga kura ya urais na ubunge hadi siku ya alhamisi huku ripoti za idadi ndogo ya wapiga kura waliojitokeza zikitolewa.

Kura hiyo imesusiwa na upinzani ambao unasema kuwa idadi hiyo ya wapiga kura inaonyesha raia hawajali na kwamba kuna uwezekano mkubwa kwamba rais Omar Al Bashir atatangazwa mshindi.
Bwana Al Bashir amekuwa mamlakani tangu mwaka 1989.
Rais wa Sudan Omar Al Bashir
Shughuli ya upigaji kura ilitarajiwa kuchukua siku tatu na kukamilika leo.
Mkuu wa tume ya uchaguzi alisema kuwa alitarajia idadi ya wapiga kura ijitokeze na kufikia asilimia 45.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment