Pages

Pages

Pages

Thursday 2 April 2015

MAAJABU: SURA YA MKE YAMTISHA MUMEWE HARUSINI

Kangu Hu akiopolewa
Duniani kuna mambo, kuna vibweka na vibwakuro pia, twende sawa, Kang Hu, mwenye umri wa miaka 33, aliwashtua wageni waalikwa siku ya harusi yake, pale alipoamua kuwaomba radhi wakiwemo familia yake na bi harusi Na Sung, mwenye umri wa miaka 30, kwa kumwambia dhahiri shahiri kuwa ana sura mbaya na hafai kuolewa.

Bwa harusi akiopolewa
Bwana harusi huyo alikanganyikiwa mara baada tu ya kumwona bi harusi wake kwa mara ya kwanza na kujaribu kujitosa majini.
Mara akaamua kutoka eneo la tukio, kwenye ukumbi wa sherehe katika mji wa Shiyan mji ulioko nchini China jimbo la Hubei na baadaye alioneka akitembea kando ya mto akiwa na mawazo meeengi,mto ambao alijirusha ndaniye mara moja.
Bwana harusi amekwisha opolewa,hoi tepe tepe.
Pal Chan Wang alisema kwamba : familia ya bi harusi ilivurugikiwa,familia ikashikwa na ghadhabu,na familia ya mwanaume yao ikafura na marafiki zake walifadhaika mnoo kwa matamshi yake .
Kang alikuwa na uchaguzi wa bi harusi amtakaye na alikuwa akilazimishwa kumuoa bi harusi huyo, ndo alipoamua kumfanyia kituko hicho.
Wapiti njia ndio waliomgundua Kang mtoni ndipo walipowaita polisi na kuharakisha kushuka mtoni kumuopoa.
Askari wakiwa mtoni tayari kumuopoa bwana harusi.
Qan Tsui, mwenye umri wa miaka25, yeye ndiye aliyepiga picha hizi anaeleza kwamba bwana harusi huyo alipojitosa mtoni alikuwa na nguo zake zote na alikuwa akielea uso ukiwa unaelekea chini kwenye maji,akiwa hajiwezi na mara nikasema anaweza kufa asipopata msaada wa haraka.
polisi walipowasili eneo la tukio,mmoja wao alijitosa mtoni na kumdaka mara moja,na mwingine aliwarushia Kamba ili wamvutie nje ya maji ya mto huo baadaye wamtoe maji yaliyoko kifuani.
CREDIT: BBCSWAHILI


No comments:

Post a Comment