Pages

Pages

Pages

Monday 20 April 2015

DAWA YA MAGUGU YAUWA WATU NIGERIA

O, Nigeriando
Shirika la Afya Duniani, WHO, linasema inavoelekea dawa ya kuuwa magugu ndio chanzo cha vifo vya watu 18 vilivyotokea kusini-magharibi mwa Nigeria, bila ya sababu kujulikana.

Katika siku chache zilizopita wakaazi katika jimbo la Ondo wamekufa saa chache baada ya kuhisi macho hayaoni sawasawa na kuumwa na vichwa.
Baadae wanazimia.
Msemaji wa WHO alieleza kuwa ukaguzi uliofanywa hadi sasa kutafuta virusi au bacteria haukugundua kitu.
Alisema kwa sasa mawazo yao ni kuwa vifo hivyo vilisa-babishwa na dawa ya kuuwa magugu.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment