![](http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/304/amz/worldservice/live/assets/images/2014/06/24/140624083853_maria_sharapova_304x171_getty_nocredit.jpg)
Maria Sharapova
Sharapova anayeshikilia nafasi ya pili kwa ubora duniani alikubali kichapo cha seti 7-6 (7-4) 6-3 kutoka kwa Daria Gavrilova anayeshikilia nafasi ya 97 kwa ubora wa mchezo huo duniani.
Katika mchezo mwingine Caroline Wozniacki, alimgaragaza Madison Brengle wa Marekani kwa seti 6-0 6-1.
Kwa upande wa wanaume Vasek Pospisil wa Canada alipata ushindi wa kishindo dhidi ya mpinzani wake Juan Martin Del Potro toka Ajentina kwa seti 6-4 7-6 (9-7)
Michezo mingine ya leo, mchezaji nambari 3 kwa ubora duniani Rafael Nadal atachuana na Nicolas Almagro, huku Andy Murray akionyeshana kazi na Donald Young wa Marekani.
CREDIT: BBC
No comments:
Post a Comment