Pages

Pages

Pages

Saturday 28 March 2015

SHARAPOVA NJE MICHUANO YA MIAMI


Maria Sharapova
Sharapova anayeshikilia nafasi ya pili kwa ubora duniani alikubali kichapo cha seti 7-6 (7-4) 6-3 kutoka kwa Daria Gavrilova anayeshikilia nafasi ya 97 kwa ubora wa mchezo huo duniani.

Katika mchezo mwingine Caroline Wozniacki, alimgaragaza Madison Brengle wa Marekani kwa seti 6-0 6-1.
Kwa upande wa wanaume Vasek Pospisil wa Canada alipata ushindi wa kishindo dhidi ya mpinzani wake Juan Martin Del Potro toka Ajentina kwa seti 6-4 7-6 (9-7)
Michezo mingine ya leo, mchezaji nambari 3 kwa ubora duniani Rafael Nadal atachuana na Nicolas Almagro, huku Andy Murray akionyeshana kazi na Donald Young wa Marekani.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment