Pages

Pages

Pages

Tuesday 31 March 2015

NDUGU KUVAANA FAINALI ZA TENISI

 
Venus Williams
 
Serena Williams

Mcheza tennis wa Marekani Venus Williams anaelekea kupambana na mdogo wake Serena Williams katika fainali za Miami Open baada ya jana kumshinda Caroline Wozniacki katika hatua ya 16 bora.

Katika mashindano hayo yanayoendelea huko Miami Marekani, Venus alimshinda mpinzani wake huyo raia wa Denmark kwa set 6-3 7-6 (7-1) katika kipindi cha dakika 98.
Awali mchezaji huyo hakuwa katika ubora wake kwa takribani miezi saba baada ya kugundulika kuwa hali yake ya kiafya kuwa si njema mnamo mwaka 2011, lakini sasa ameshinda michezo saba kati ya nane aliyocheza dhidi ya wachezaji walio katika viwango vya kumi bora. Wakati dada akifanya hayo Serena alimgaragaza Svetlana Kuznetsova kwa ushindi wa set 6-2 6-3 kuingia katika robo fainali.

CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment