Pages

Pages

Pages

Friday 13 March 2015

MWALIMU MKUU AJIGEUZA MTENDAJI, MGAMBO

Na Hastin Liumba, Kaliua

WANANCHI wa kata ya Zugimlole wilaya ya Kaliua mkoani Tabora wamemkataa mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Zugimlole Azbert Kamala kwa hatua yake ya kujigeuza afisa mtendaji wa kata na askari mgambo na kushirikiana na askari mgambo wengine kukamata wahalifu.


Hayo yalibainika kwenye mkutano wa hadhara kufuatia ziara ya mbunge wa viti maalumu (CUF) Magdalena Sakaya.

Wananchi hao walimueleza mbunge huyo kuwa wamefikia mahali wamechoshwa na mwalimu mkuu huyo licha ya kutoa taarifa serikalini lakini hadi sasa mwalimu yupo kwenye kituo chake cha kazi.

Selegedu Dushonde mkazi wa kata ya Zugimlole alisema mwalimu mkuu huyo aliwahi kumkamata mchungaji wa n g`ombe zake 20 Mayala Joseph (18) mwezi April 2014 na kumwambia ni mtoro wa shule.

Alisema wakati anakamatwa kwa kushirikiana na baadhi ya mgambo walimchukua hadi kwa mama yake mzazi na kisha walilazimisha wapewe sh 500,000 fedha ambazo walipewa ili Joseph aachiwe na kesi ifutwe.

Alisema walilifikisha kwa mwenyekiti wa kitongoji Jidagina Luboke na mratibu kata elimu Siphela Charles.

Hata hivyo alisema mwenyekiti wa kitongoji alilazimika kumuita mwalimu mkuu huyo lakini aligoma hadi alipokamatwa na kulala kituo cha polisi Kaliua siku mbili.

Alisema siku chache alikamatwa na polisi bila kosa na kuwekwa ndani ambapo mama yake mzazi alilazimika kutoa sh 300,000 ana aliachiwa toka kituo cha polisi.

Hata hivyo hadi sasa licha kuachiwa bado mwalimu huyo hajachukuliwa hatua yoyote na ameachiwa na kuendelea kutanua na kutoa vitisho kuwa yeye ni serikali hakuna wa kumbabaisha.

Wakichangia kwenye mkutano huo baadhi ya wananchi walimueleza Sakaya afanye awezavyo mwalimu huyo aondoke kijijini kwao vinginevyo watachukua hatua ya kumtoa mbio.

‘Mkuu tusaidie tuondokane na hii kero mwalimu mkuu huyo hatumtaki kijijini kwetu……nenda katusemee kwa mabosi wake aondoke hapa tutamshughulikia tumechoshwa naye.’walisema.

Mwalimu mkuu Azbert Kamala alipotwafutwa shuleni na nyumbani kwake hakupatikana ambapo gazeti hili lilifanya jitihada na kufanikiwa kuonana naye lakini hakutoa ushirikiano na aligoma kuongea wala kukanusha tuhuza hizo.

Mbunge wa viti maalumu (CUF) Magdalena Sakaya aliwaeleza wananchi hao suala hilo analichukua na mwalimu mkuu huyo ataondoka kwani amesikia kilio chao.

‘Ndugu zangu nimewasikia huyo mwalimu ataondoka nitakula naye sahani moja kuhakikisha hatua za kinidhamu zinachukua mkondo wake……hatuwezi kuvumilia wezi kama hawa alikuja kufundisha au kuwa mgambo.”alisema.

No comments:

Post a Comment