Pages

Pages

Pages

Saturday 14 March 2015

MVUA YALETA MAAFA ANGOLA, 60 WAFA MAJI



Watu 60 wakiwemo watoto 35 wamefariki dunia kufuatia mvua nyingi iliyonyesha nchini Angola.

Miongoni mwa waliokufa katika mvua hiyo iliyoshesha katika mji wa bandari wa Lobito ni watoto 35.
Shirika la habari la nchi hiyo -ANGOP-limesema kwamba katika baadhi ya maeneo wafuriko yalifikia kipimo cha mita tatu na kuharibu nyumba kadhaa.
Wafanyakazi wa uokoaji wanaendelea kutafuta watu walionusurika na janga hilo.
Sehemu kubwa ya Angola imekumbwa vibaya na mvua nyingi zinazonyesha tangu Januari, katika mji mkuu wa Luanda zaidi ya nyumba 130 zimeharibiwa na mvua hiyo.
CREDIT SOURCE: BBC

No comments:

Post a Comment