Pages

Pages

Pages

Wednesday 31 December 2014

MTOTO WA MIAKA MIWILI AUA MAMA YAKE


Maafisa nchini Marekani wanasema kuwa mtoto mmoja mdogo mvulana wa miaka miwili amempiga risasi kimakosa mama yake mzazi na kumuua ndani ya duka moja kubwa la uuzaji bidhaa la Wal-Mart.

Maafisa wa usalama wanasema bunduki iliyotumika iliyokuwa imefichwa ilichomoka wakati mvulana huyo alipokaribia na kuligusa begi la mkononi la mama yake mwenye umri wa miaka 29.
Tukio hilo limetokea katika mji wa Hayden, katika jimbo la Idaho.
Msemaji wa Kaunti hiyo anasema mwanamke huyo alikuwa na kibali cha kumiliki silaha.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment