Pages

Pages

Pages

Saturday 27 December 2014

POLISI ACHOMWA MKUKI NA WAVAMIZI MGODINI

Kamanda wa Polisi wa Tarime Rorya, ACP Lazaro Mambo

Na Samson Chacha, Tarime
Askari polisi Deogratius wa Kituo cha Polisi, Kinesi Wilayani Rorya mkoani Mara, amechomwa mkuki na wananchi waliovamia mgodi wa dhahabu wa ACACIA North Mara kwa lengo la kupora mawe.


Kamanda wa Polisi wa Tarime Rorya, ACP Lazaro Mambo, alisema jana kuwa, askari huyo alijeruhiwa na kundi la watu zaidi ya 2,000 lililovamia kwenye mgodi huo Jumanne ya wiki hii.

Alisema wavamizi hao walikuwa na silaha mbalimbali za jadi.

Alisema mara baada ya kuingia ndani ya mgodi huo, watu hao walifanya vurugu kwa kuwashambulia askari na walinzi waliokuwa wakilinda mgodi huo.

Alisema lengo la watu hao lilikuwa ni kupora mawe ya dhahabu yaliyokuwamo.

Alisema jeshi lake likishirikiana na walinzi wa mgodi huo uliopo Nyamongo Wilayani Tarime, lilifanikiwa kuwaondoa wavamizi hao kwa kutumia mabomu.

Alisema katika tukio hilo, askari huyo alijeruhiwa kwa mkuki na amelazwa katika hospitali ya Shirati kwa matibabu.

Alisema hadi sasa wanawashikilia watu sita kwa tuhuma za kuvamia na kujeruhi baadhi ya askari mgodini humo.
Alisema watu hao watawafikishwa mahakamani wakati wowote uchunguzi utakapokamilika.
 
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment