Pages

Pages

Pages

Wednesday 5 November 2014

KIONGOZI WA DINI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI KENYA

Masjid Musa, Mombasa
Watu wasiojulikani kwenye mji wa pwani nchini Kenya, Mombasa, wamemuua kwa kumpiga risasi kiongozi mashuhuri na mwenye msimamo wa wastani wa dini ya Kiislamu.

Sheikh Salim Bakari Mwarangi ambaye ni mwanaharakati wa kampeni dhidi ya itikadi kali alipigwa risasi wakati alipokuwa akirudi nyumbani kutoka msikitini jumanne usiku.
Viongozi sita wa dini ya kiislamu badhi yao wenye itikadi kali na wale walio na misimamo ya wastani wameuawa mjini Mombasa tangu mwaka 2012.
Eneo la pwani ya Kenya lenye Waislamu wengi limekumbwa na misururu ya mashambuli ya mabomu yanoyoaminika kutekelezwa na watu walio na uhusiano na kundi la Al Shabaab lenye makao yake nchini Somalia.
CREDIT: BBC

No comments:

Post a Comment