Pages

Pages

Pages

Wednesday 29 October 2014

RAIS MALINZI KUFUNGUA KOZI YA FUTURO III

Jamal Malinzi

Na Mwandishi Wetu
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi kesho (Oktoba 29 mwaka huu) anafungua kozi ya ukufunzi wa waamuzi ya FUTURO III ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).


Hafla ya ufunguzi wa kozi hiyo inayoshirikisha zaidi ya waamuzi 40 wakiwemo baadhi ya wale ambao bado wanachezesha mpira wa miguu kutoka nchi mbalimbali za Afrika itafanyika saa 4 asubuhi kwenye hoteli ya Holiday Inn, Dar es Salaam.

Kati ya hao, washiriki wanane wa kozi hiyo inayoanza kesho hadi Novemba 3 mwaka huu chini ya wakufunzi wa FIFA wakiongozwa na Carlos Henriques ni kutoka Tanzania.

Washiriki kutoka Tanzania ni Emmanuel Chaula, Joan Minja, Josephat Bulali, Paschal Chiganga, Ramadhan Ibada, Richard Kayenze, Samuel Mpenzu na Soud Abdi.


No comments:

Post a Comment