Pages

Pages

Pages

Friday 3 October 2014

MAHAKAMA YAPIGA STOP TAMASHA LA 'BANG BANG BEAR FEST’ JUMAMOSI HII, LIMEKIUKA SHERIA ZA HAKI MILIKI



Dar es Salaam, Okt 3, 2014
Mahakama ya hakimu mkazi Kinondoni jijini Dar es Salaam imezuia kufanyika kwa tamasha lililopewa jina ‘Bang Bang Bear Fest’ lililokuwa linatarajiwa kufanyika Jumamosi hii.


Uamuzi wa mahakama hiyo umetokana na malalamiko yaliyotolewa na Bongo5 Media Group ambao wanamiliki wazo halisi la tamasha la aina hiyo liitwalo Dar es Salaam Bear Fest.

Kwa hali hiyo mahakama hiyo imetoa amri ya kusitishwa mara moja kwa ‘Bang Bang Bear Fest’ lililokuwa lifanyike October 4 kwenye viwanja vya Posta Kijitonyama, Dar es Salaam pamoja na kulipa hasara yoyote iliyotokana na kuingiliwa kwa haki miliki hiyo.





No comments:

Post a Comment