Kwa siku ya pili mfululizo kumekuwa na mapambano katika Mji wa Missouri nchini Marekani kufuatia kifo cha kijana mmoja mweusi, Michael Brown, ambaye alipigwa risasi na polisi katika Kitongoji cha St Louis siku ya Jumamosi.
Mkuu wa polisi wa kitongoji cha watu weusi cha Ferguson, Tom Jackson amesema kwamba polisi walitumia gesi na risasi za bandia ili kuwatawanya watu waliokuwa wamefurika karibu na jengo ambalo liliteketezwa kwa moto siku ya tukio ambapo maduka yaliporwa bidhaa na magari yaliharibiwa vibaya.
Ni wakati huo wa utumiaji wa gesi na risasi bandia ndipo raia walipoamua kuwarushia mawe polisi,polisi nao wakajibu mapigo kwa kuwarushia risasi raia hao.
Kijana Michael Brown,alipigwa risasi kadhaa alipokuwa amening'inia kwenye gari ya polisi, na kufuatia tukio hilo FBI wanachunguza endapo kuna uvunjifu wa haki za binadamu katika tukio hilo la kuuawa kwa kijana Michael Brown.
BBC
No comments:
Post a Comment