Pages

Pages

Pages

Sunday 10 August 2014

NDEGE YAANGUKA NA KUUA 40 IRAN

Ndege iliyoanguka nchini Iran

Ndege moja iliokuwa na abiria 40 imeanguka mjini Tehran nchini Iran.
Runinga ya taifa la Iran imesema kuwa abiria wote wamefariki .
Ndege hiyo inayojulikana kama Iran 141 ilitengezwa nchini Iran kupitia teknologia ya Ukraine.Ndege hiyo ya kampuni ya Taban Air imeripotiwa kuanguka katika makaazi baada ya kupaa kutoka uwanja wa ndege wa Mehrabad Maghribi mwa mji wa Tehran.
Uchunguzi umeanzishwa kuhusu ni nini kilichosababisha ajali hiyo.

Iran imekabiliwa na ajali kama hizo katika siku za hivi karibuni kutokana na ndege zake zilizozeeka mbali na marekebisho mabaya inazozifanyia.
BBC/SWAHILI

No comments:

Post a Comment