Pages

Pages

Pages

Sunday 20 July 2014

WAASI SUDAN KUSINI WAUTEKA MJI WA NASIR

Wanajeshi wa serikali ya Sudan kusini wapiga doria.
Waasi nchini Sudan kusini wanasema kuwa wameuteka mji muhimu wa Nasir katika jimbo la upper Nile.
Wanasema kuwa wameuteka mji huo baada ya kushambuliwa na vikosi vya serikali.
Jeshi la Sudan Kusini limesema kuwa vita vinaendelea katika mji huo,ambao waasi wamekuwa wakishambulia tangu siku ya jumamosi.
Msemaji wa jeshi amesema kuwa huenda huo ukawa mwisho wa makubaliano ya kusitisha vita yaliotiwa sahihi mnamo mwezi May.

Mji wa Nasir ulikuwa makao makuu ya mda ya ya kiongozi wa waasi Riek Machar ,ambaye alihudumu kama makamu wa rais wa Sudan kusini kabla ya kutofautiana na rais Salva Kiir.
BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment