Pages

Pages

Pages

Tuesday 1 July 2014

ISRAEL YASEMA HAMAS ILIWAUA VIJANA WAKE

Vijana wa Israel waliokutwa wameuawa

Msemaji wa jeshi la Israel amesema kuwa miili hiyo ilikuwa chini ya miamba iliopo kwenye mji wa west Bank wa Hebron.
Israel imepeleka vikosi vyake katika kijiji cha Palestina cha Hal-hul.
Netanyahu amelilaumu kundi la Wapalestina la Hamas, na akaahidi kulipiza kisasi.Katika kikao cha dharura cha mawaziri ,waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema vijana hao walitekwa na kuuawa katika mauji aliyosema yamefanywa na wanyama.
Benjamini Netanyahu
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu

Hamas imekana kuhusika na mauaji hayo kupitia mshauri rasmi wa rais wa Palestina Mahmoud Abbas -Abdallah Abdallah.

Mwandishi wa BBC aliyeko mashariki ya kati anasema milio ya mashambulizi ya ndege za Israeli imesikika kote katika ukanda wa Gaza .
Kulikuwa na tetesi kuwa Israeli ingeileng maeneo ya Hamas baada ya kikao chake cha mawaziri cha usalama .
Mji wa Gaza umesalia kuwa ngome kuu ya Hamas na ofisi zake katika eneo hilo zimekuwa zikivamiwa katika kipindi cha zaidi ya wiki mbili na nusu.

vifo vya karibu wapalestina watano vimeripotiwa na mamia ya wapalestina wamekamatwa.
BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment