Pages

Pages

Pages

Friday 11 July 2014

FIFA YAIFUNGIA NIGERIA MICHUANO YA KIMATAIFA, KISA SERIKALI YAINGILIA MASUALA YA MPIRA


Shirikisho la Soka la KImataifa (Fifa), imeifungia Nigeria kushiriki michuano ya kimataifa.
Fifa imeifungia Nigeria kwa muda usiojulikana kutokna na serikali kuliingilia shirikisho la soka la nchi hiyo NFA.
Maana yake Nigeria pamoja na klabu zake zote za soka Nigeria hazitashiriki michuano ya kimataifa.

Fifa imeamua kuchukua uamuzi huo baada ya serikali ya Nigeria kuusimamisha uongozi wa NFA kwa madai kwamba ulifanya madudu wakati timu ya taifa ya nchi hiyo ikishiriki Kombe la Dunia.

Lakini Fifa ikaonya kwamba si sahihi kuingilia masuala ya soka, serikali ya Nigeria haikutekeleza onyo hilo la Fifa kwa kulisikiliza na kulifanyia kazi. Mwisho shirikisho hilo limepitisha uamuzi wa kuifungia Nigeria.

CHANZO MPENJA BLOG

No comments:

Post a Comment