Twitter Buzz

....

....

...

...

IMETOSHA!

IMETOSHA!

Featured post

KIJANA GOZBERT BWELE ALIVYOMPAGAWISHA MAKAMU WA RAIS WA HISPANIA MJINI NANSIO

Makamu wa rais mstaafu wa Hispania, Mama Maria Teresa Fernandes De la Vega alishindwa kujizuia na kwenda kumtuza mtoto Gozbert ...

Sunday, 22 June 2014

WENGI WAUAWA NIGERIA

Waumini kanisani wakiomba wasichana wa Chibok waachiliwe huru
Inafikiriwa kuwa watu kadha waliuwawa katika mashambulio yaliyofanywa na wale wanaoshukiwa kuwa wapiganaji Waislamu kaskazini mwa Nigeria hapo jana.
Wakaazi wa huko wanasema wapiganaji wa Boko Haram walikuwapo kwa saa sita, wakiuwa watu na kuchoma moto vijiji.
Inasemekana kati ya waliouwawa ni askari wa usalama.
Baadae wanajeshi na ndege zilipelekwa katika eneo hilo na mtu mmoja aliyeshuhudia tukio hilo, anasema maiti za wapiganaji kadha zimekutikana nje ya vijiji.
Mashambulio hayo yalifanywa karibu na Chibok ambako wapiganaji waliwateka wasichana wa shule zaidi ya 200 mwezi Aprili.
BBC

No comments:

Post a Comment