Pages

Pages

Pages

Monday 5 May 2014

MVUA YAMUWEKA KINANA DAKIKA 20 ANGANI


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishuka kutoka kwenye ndege ya kampuni ya Flightlink kwenye uwanja wa Ndege wa Zanzibar baada ya kukaa angani kwa dakika 20 zaidi ya muda uliopangwa kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya na mvua kubwa kunyesha.Katibu Mkuu amewasili Zanzibar kwa ajili ya mkutano wa hadhara utakaofanika kwenye viwanja vya mikutano vya Kibanda Maiti.


Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye akishuka kutoka kwenye ndege ya kampuni ya Flightlink kwenye uwanja wa Ndege wa Zanzibar baada ya kukaa angani kwa dakika 20 zaidi ya muda uliopangwa kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya na mvua kubwa kunyesha. Katibu Wa NEC ameongozana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.


Mvua kubwa ikinyesha Zanzibar ambapo CCM inatazamiwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara.


Mitaa mbali mbali ikiwa imefurika maji kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Zanzibar.


CHANZO FULL SHANGWE

No comments:

Post a Comment