Utabiri wa Maalim Hassan Yahya Hussein ambaye ni mrithi wa aliyekuwa Mnajimu Mkuu Afrika Mashariki na Kati Sheikh Yahya Hussein alioutoa tarehe 13/1/2013 mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu ushindi wa aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya Mh. Raila Odinga katika uchaguzi mkuu uliofanyika march mwaka huu umeota mbawa kutokana na ushindi alioupata Uhuru Kenyatta katika uchaguzi huo.

Kati ya mambo aliyoyatabiri ni Nyota za utendaji kazi wenye ufanisi serikalini za mawaziri; Dk. Harrison Mwakyembe (Uchukuzi), John Magufuli (Ujenzi) na Balozi Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), zilimetabiriwa kuwa zitazidi kung’ara na kuungwa mkono na wananchi.Kadhalika, Rais Jakaya Kikwete, akitabiriwa pia kufanya maamuzi magumu yatakayoishangaza dunia, katika mwaka huu 2013.

Source: NIPASHE tarehe 14/1/2013.